Mikumi
Hifadhi ya Taifa ya Mikumi iko Mkoani Morogoro kati ya Milima ya Uluguru na safu ya Lumango. Hifadhi hii ni ya nne kwa ukubwa nchini Tanzania na ni karibu sana kutoka Dar es Salaam katika barabara kuu iendayo Mbeya kupitia Iringa.
Watalii wengi wanaotembelea Hifadhi ya Mikumi wanapenda kuona wanyama maarufu “The Big Five”. Wanyama hao ni Chui, Simba, Faru, Tembo na Nyati. Idadi kubwa ya “mabwawa boko” huwawezesha watalii kuwasogelea karibu zaidi viboko ambao hupenda sana kucheza kwenye tope.
Kwa kuwa Hifadhi ya Mikumi iko karibu sana na Jiji la Dar es Salaam wageni wengi na baadhi ya wafanyabiashara hupendelea kwenda huko kwa mapumziko mafupi hasa wale ambao hawana muda wa kwenda mbali kwa shughuli za kitalii.
Mikumi inapakana na Milima ya Udzungwa pamoja na Mbuga ya Wanyama ya Selous na kwa pamoja hutengeneza ukanda maalum wa utalii.



Je ulikuwa wajua?


