Saadani
Saadani, ambayo hivi karibuni imepandishwa hadhi na kuwa Hifadhi ya Taifa, ni kiunganisho kizuri kati ya ufukwe wa bahari na nchi kavu na iko kilometa 70 tu kaskazini mwa mji wa Bagamoyo. Sehemu hii inafikika kwa urahisi kwa barabara toka Dar es Salaam na inatembelewa sana na watalii hasa wale wanaopenda kujipumzisha katika fukwe za bahari kati ya Dar es Salaam na Tanga.
Mto Wami ambao unapita kati kati ya Hifadhi ya Saadani na kumwaga maji yake katika Bahari ya Hindi ni makazi mazuri ya viboko, mamba, flamingo na aina nyingi ya ndege wakubwa. Makundi ya tembo wanaonekana wakiranda randa ufukweni karibu sana mto hasa majira asubuhi. Kitu cha pekee cha kuvutia katika Hifadhi ya Saadani ni kuona tembo wakifurahia kucheza na kasa katika povu la mawimbi ya bahari.



Je ulikuwa wajua?


